Habari
PROF. MKUMBO ASHIRIKI KONGAMANO LA UWEKEZAJI NA BIASHARA KATIKA MJI WA NANTONG, NCHINI CHINA LILILOKUTANISHA WAWEKEZAJI NA WAFANYABIASHA WA SEKTA YA VIWANDA VYA NGUO
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo, leo ameshiriki Kongamano la Uwekezaji na Biashara katika Mji wa Nantong, nchini China, ambalo limekutanisha zaidi ya wawekezaji na wafanyabiasha 200 wa Sekta ya Viwanda vya nguo
Kongamano hilo ni kuhamasisha uwekezaji utekelezaji wa ahadi iliyotolewa na Rais wa China, Xi Jinping, wakati wa mkutano wa FOCAC mwaka 2024 , ambapo aliahidi kutoa kiasi cha dola bilioni 50 kwa ajili ya kuwezesha utekelezaji wa maeneo 10 ya ushirikiano kati ya nchi ya China na nchi za Afrika iliwemo kuwezesha uwekezaji.
