Habari
Waziri Mhe. Prof. Kitila Mkumbo asaini Mikataba ya Ushirikiano baina ya Tanzania na India katika sekta mbalimbali.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji Prof. Kitila Mkumbo (Mb.) akiwa na Waziri wa Mambo ya Nje wa India, Mhe. Dkt. Jaishankar wakionesha mikataba 15 ya ushirikiano baina ya nchi hizi mbili katika sekta ya elimu, kilimo, uchumi wa bluu, ulinzi, usalama wa bahari, maji, usafi, afya, teknolojia ya Habari na mawasiliano, biashara na uwekezaji katika hafla iliyofanyika New Delhi Nchini India.